Tuesday, February 5, 2013

FAHAMU BAADHI YA TABIA ZA MWANADAMU


 

Na; Cyprian Sallu
Wapendwa katika maisha ya mwanadamu lazima kuwepo na mambo mbalimbali ambayo yanaendana na maisha yake pamoja na mazingira ili kukamilisha mfumo kamili wa maisha ya kiroho na kimwili.Hayo yote yaliyotajwa hapo yanaitwa TABIA.Tabia huleta picha kamilsi ya mtu na mfumo wake wa maisha  vilevile hujulikana haraka sana kwa jamii inayozunguka eneo husika au mtu Fulani kwa sababu wao ndio wanao kuona siku zote.Mara nyingi tumekwepa sana kutazama tabia zetu na tukajishughulisha sana na mambo ya kanisa jambo ambalo husababisha kutokea kwa dhambi.Lakini Tabia ya mtu si rahisi kubadilika  mpaka Mungu mwenyewe ambadilishe na amshuhudie kuhusu tabia yake.
Mtume Paulo alipewa neema na Mungu katika kujua tabia ya wakristo huko Effeso na Korintho alibahatika kufahamu tabia  na mwenendo wa wakristo katka kila kanisa  kupitia njia ya roho,mafunuo .na shuhuda ndio maana alisema, ‘’Sikuweza kusema nanyi kama watu wenye  tabia ya rohoni bali kama watu wenye tabia  ya mwilini kama watoto wachanga katika kristo’’.Alieleza hivyo kwa mtazamo wa tabia zetu sisi wanadamu na maisha yetu kwasababu lazima kila mtu aishi chini ya mwongozo wa neno  la mungu ili kwamba Tabia zetu ziwe za kiroho na kuwa Baraka kwa wenzetu sio vikwazo.
Kutokana na hayo tabia ikajigawa katika makundi mawili  TABIA  NZURI NA TABIA MBAYA .Lakini  pia katika hayo makundi  mawili yanajumuisha aina zifuatazo za Tabia  katika maisha ya Mwanadamu  ambazo zinahitaji utashi katika kufanya uamuzi na kuishi kwa kuepuka vikwazo nza mitego ya shetani.

Aina za Tabia:

01.Tabia ya Kurithi:

Aina  hii ya Tabia ni vigumu kuifahamu na kuitambua endapo hutakuwa mfuatiliaji na usipo vunja laana za ukoo maana hutokana na kurithi aidha kwa kupitia majina ya kurithi kutoka kwa vizazi vyetu.Katika kurithi kunaweza kuwa na Tabia nzuri au Tabia mbaya , hivyo basi ni vizuri kila mzazi kuwa makini na kufuatilia kuhusu majina na vitu ambavyo wanarithisha watoto wao.Mfano wa tabia ambazo zinaweza kurithiwa,Uchawi,Uongo,Kiburi,Hasira na Nyingine nyingi.
     Kuabudu imani za kishirikina na hata kurithishwa mikoba ya uchawi ni mmoja ya tabia za shetani                                                                                                 
Umakini unahitajika katika kuepuka aina hii ya Tabia kwasababu jamii yetu imekuwa na utamaduni wa kurithishana hasa majina  Mfano, Mtoto anaweza kuzaliwa akapewa jina la babu yake  lakini wazazi bila kufahamu na kufuatilia historia ya mwenye jina wajikuta wamempa mtoto jina bila kuvunja laana na kulitakasa jina lhilo upya ili mtoto asiweze kurithi hizo tabia  za babu yake.Ni jambo gumu sana kwa mtu asiyeamini na kufuatilia maandiko ya neno la mungu kwasababu laana imezungumzwa katika biblia kuwa inaweza kumktesa mtu bila yeye mwenyewe kujua,unaweza kuona mtu hafanikiwi au kila akifanya jambo haliendi vizuri anakimbilia kwa waganga wa kienyeji akienda kusafisha nyota kumbe siri imejificha kwenye laana ya kurithi jina la mtu wa zamani .Hivyo basi ni  vema kila mmoja kufuatilia asili ya jina lake na historia ya ukoo wake ili kuepuka kuwepo kwa tabia za kurithi bila yakujua.

02.Tabia ya Kuiga
Tabia hii inakundi kubwa la watu wambao wameathiriwa kwasababu ya mabadiliko ya mfumo wa maisha na utandawazi hasa vijana ambao  hupenda sana kuiga Tabia ,mienendo na mifumo ya maisha bila kufahamu hapo baadaye.Mara nyingi watu huiga kutoka kwa marafiki,ndugu na jamaa kwa lengo la kuwaridhisha au kujiridhisha wenyewe kwamba wanaenda na wakati lakini hawajui nini madhara ya kuiga.

1 Waebrania 13;17, anatufundisha Tabia zitupasazo kuwa nazo kuwa tuwa tii wale wanaotuongoza tena tuwaige na kufuata mienendo yao mizuri na ndio maana wakristo wengi wanabatizwa majina ya watakatifu waliopita Mfano , Petro,Musa,Paulo,Mathayo na wengine wengi.Vijana wengi wameingia katika kundi  hili la kuiga ilikuonekana wakotofauti na wengine lakini sababu kubwa ni kutokulifahamu neno lamungu pamoja na historia ya ujana wa Yesu,hivi leo kijana anaeokoka huonekana mshamba  lakini kijana aliyejiingiza kwenye kuiga mambo ya kigeni kama vikundi vya wacheza disco,walevi na wahuni anaonekana wa maana kuliko Yule aliyeko kanisani.Ni wakati wa kila kijana kujitambua na kijijengea tabia nzuri yenye misingi na misimamo ya kiroho ili kujiwekea heshima kwenye jamii na maisha yake ya kiroho yakiwa ushuhuda kwa kuutumia ujan wake vizuri bila kuiga mambo yasiyo na maana mbele za Mungu .
        Ulevi na ndoa za jinsia moja ni moja wapo ya Tabia ambazo maranyingi mwanadamu anaiga kutoka kwa mwingine
Hata jamii nzima ya kitanzania imeanza kuiga utamaduni mbovu kama ndoa za jinsia moja ambazo hazipo kwenye neno la Mungu na ni tabia ya kishetani.  Ni jukumu la watumishi wa Mungu na wazazi kuwajengea watoto na kurekebisha tabia ya kuiga ,pia kuna baadhii ya watumish nao wanaiga mambo jambo ambalo linahuzunisha na linapoteza heshima yao katika utendaji wao kwasababu hakuna Nabii wala Mtume mwenye historia ya tabia hii ya kuiga. Hivyo ni jukumu la kila mmoja kujitengenezea na kufuata tabia za kiutauwa na kuenenda  akiwa ongozwa na roho mtakatifu ili kuepuka kuiga mambo yasiyoendana na ukristo pamoja na maagizo ya Mungu wetu vile vile ni heri kuiga mambo mazuri kuliko mabaya

03:Tabia Ya Kuambukizwa:
Hii ni Tabia ya mwilini,katika amri zote mwanadamu anatakiwa ajihadhari na mawasiliano ya mtu yeyoytekidamu  ndio maana imeandikwa dhambi zote tunazofanya ni makosa lakini dhambi  ya  uzinzi na uasherate ni dhambi ya damu kuna  kuambukizana tabia kuna kuambukiza hali mbaya .Enzi hizo wayahudi wakikuta mtu anazini lazima apigwe mawe afe maana wamekwisha kuambukizana uzinzi natolea mfano uzinzi na uasherati kwasababu ni dhambi ambazo zinaambukizwa kwa kushawishiwa  mtu hawezi kufanya akiwa peke yake na zipo Tabia nyingi za kuambukizwa hivyo ni jukumu mkristo kutambua .
Ukahaba ni mmoja wapo ya tabia ya kuambukizwa












Madhara ya tabia hii inaweza kukufanya ubaki pale pale kimaendeleo unapoambukizwa dhambi au tabia yoyote ambayo sio nzuri ni vigumu kutoweka katika mfumo wako wa maisha ,mara nyingi epuka kujichanganya kwenye makundi ambayo hayana tabia kama yako kwasababu kinga ni bora kuliko tiba hivyo jikinge juu ya watu wenye uwezekano wa kukuambukiza tabia mbaya .                                                              Hizo ni baadhi ya Tabia za wanadamu tulio wengi ambao wakati mwingine tunaifanya mioyo yetu kuwa migumu kwa kutokuiga mwenendo wa mungu aliyetuumba na kuacha kuzifuata amri zake.Wakati mwingine tuna chelewa kupokea ahadi za mungu kutokana na Tabia zetu kutokumpendeza yeye katika  2 Petro2 neno linasema kwamba  bwana hachelewi kutimiza ahadi zake na anaiona Tabia yetu sisi lakini anatuvumilia na kutufundisha kupitia neno lake kuwa kama tabia zetu sio njema tufanye toba ya kweli kwani tukifa katika tabia mbaya tutaingia katika hukumu.Ni lazima kila mmoja achuchumilie kuishi maisha ya utauwa wa mungu na kujitahidi kuondoa Tabia za mwilini ambazo zimepelekea kwa wakristo wengi kuyumba katika huduma walizoitiwa na mungu.

Ili uwe na tabia nzuri au njema lazima upambane vizuri juu ya roho na mwili maana roho hushindana na mwili maana wakati mwingine roho inaamsha tama au vitu na tabia ambazo mwili hauzitaki lakini mara nyingi wakristo tumeshindwa kufanya maamuzi yaliyo sahihi na kufuata tama za mwili na kuwa maajenti wa shetani bila kujua  kutokana na kuingiwa na roho chafu kwasababu ya Tabia zetu tulizo nazo.Shetani amekuwa macho akitazama Tabia zetu hivyo akiona tabia yako mbovu anaingia kwa urahisi  vile vile jinsi tabia  yako ilivyo kutakufanya uingie jehanamu au uzimani.

Dawa Ya Tabia Mbaya:
Tabia mbaya inabadilishwa na Neno la Mungu likiingia ndani ya moyo wa mwanadamu linasafisha na kuondoa roho ngeni na Tabia zake jambo  ambalo hutokea baada ya wewe mwenyewe kuamua kumpa Yesu maisha yako na kukubali kuwa neno la Mungu ni dawa na suluhisho la shida zako.
Yesu ni dawa ya tabia mbaya ukiamini na kufuata neno lake...
Wito Kwa Wote;Wakati  wote tukumbuke mwanadamu aliumbwa na Mungu hivyo ni lazima afanye na kufuata mapenzi na amri za mungu ili asimuudhi tena tusiweke ushabiki katika kumtafuta mungu na ufalme wake lakini kwa wakati huu Wainjilisti,Wachungaji Na Wanaojiita Manabii wamekuwa na Tabia ya kujitwalia utukufu kwamba wao ndio wanamtuma Mungu na wanaponya wagonjwa, kutoa pepo kwa nguvu zao jambo ambalo halileti picha nzuri kwa watu mnao waongoza pia kuibua kiburi cha imani kati ya dhehebu na dhehebu.Inatupasa kutumika kwa moyo na kujishusha mbele za Mungu kwa kufuata maagizo na amri zake tuwaze mawazo mazuri ambayo yatatufanya tuwe na Tabia nzuri na Mungu atapata nafasi ya kukaa kwetu kutokana na mwenendo wetu mzuri .

2 comments:

  1. nime farijika sana sana na maelezo kupitia ukurasa huu Mungu awabariki mzidi kutupatia majibu ya maswali inayo umiza moyo na kutesa akili pasipo kujua wapi tupate ushauri na nini kufanya kuepuka dhambi

    ReplyDelete
  2. If Jesus made light of our life nobody will restrict the stages we made

    ReplyDelete