Tuesday, March 26, 2013

HATUA MUHIMU ZA KUKUA KIROHO


CHUKUA HATUA

MWINJILISTI  PAUL
Joshua 3:1-5 Joshua anawaambia wana wa Israeli kuchukuwa hatua ili kuweza kukabili safari  iliyokuwa mbele yao kwa kuwa  wanatakiwa wajitakase  ili waweze kuanza safari.ili uweze kufanikiwa ni lazima uchukue hatua ya kutenda au kukabili jambo husika ambalo unatalaji kulifanya,hivyo tunatakiwa tuchukue hatua katika neno ili tuweze kushinda vita vinavyo tukabili ,na Mungu anatusubili sisi aone kama tunatii neno lake kwa kuchukua hatua ili aweze kushusha Baraka zake juu yetu.
Kutoka 2:11-15 Jitahidi kuangalia hali uliyokuwa nayo  kisha angalia yale unayoyafanya  kama kweli yanaendana na neno la Mungu linavyotuonya na kutufundisha,na kama sivyo  basi chukua hatua ya kujirekebisha ili Mungu akutendee,wakristo wengi wanajifariji  kwa kuomba maombi marefu, kuhudhulia  kwenye ibada kila siku,lakini wanasahau kuwa Mungu anapendezwa na wanaotii neno lake na kukubali kutubu,kwa kughaili na kuacha maovu na kutenda mema.Kutoka 3:6 acha kujifariji kwa kuigawa dhambi ukidhani kuna kubwa na ndogo,elewa  kwa Mungu zote ni dhambi kwa kuwa zinampeleka mtu jehamu.Kutoka 5:1 licha kuwa  utachukuwa hatua  sio  kwamba mambo yatakuwa mazuri  hapana, inawezekana yakawa magumu sana ,kama ilivyokuwa kwa Musa na Haruni wakati Mungu anasema nao juu ya kwenda kwa Farao kuomba kibali cha wana wa Israeli  kwenda kumwabudu Mungu wao.kutoka 5:1-12 tunapochukuwa hatua bwana anajidhibitisha kwetu,zipo hatua zinazotufaa sisi tuzichukue ili kuweza kupona.
·                            Chukua  hatua ya kuliamini neno la Mungu.Kutoka 14:13-16,wakristo walio  wengi wanashidwa kwa kuwa wanakuwa mafundi wa kusikiliza na kuandika mafundisho yote yanayofundishwa,lakini  ndani yao kumejaa mwalakini na kutoamini kuwa maneno  yanayosemwa au ahadi zilizotolewa na Mungu kuwa ni kweli ,tunakuwa wagumu wa kuamini  tunasubili mpaka tuone ndipo tuamini ,yapo mengine hatutapokea endapo hatutaruhusu  kuamini ndani yetu.
·                       Chukua hatua ya kutenda.yapo mafundisho ya Mungu ambayo yanatufundisha  kuamini neno la Mungu ili tuweze kupokea Baraka ,lakini waliowengi ndani yetu tumekuwa na mashaka juu ya kile ambacho tunakiomba na matokeo yake watu hawapokei kwa kuwa ndani yao yamejaa mashaka  mengi.Musa anaambiwa na Mungu juu ya kuwaongoza wana Israeli afanye tendo la imani la kupiga fimbo juu ya bahari na Musa alipochukua hatua bahari iligawanyika na wakapita salama,je? endapo angekuwa na mashaka wangevuka? Matendo 12:1…,Hesabu 13:1-3
·                      Chukua hatua ya kuhakikisha  kile unachoambiwa.katika nyakati hizi  tulizo nazo ni ngumu na mbaya sana kama hatutachukuwa hatua  za kumkariba Mungu ili atusaidie,kwa sasa  wapo watu wanaojiita kuwa ni manabii na  mitume na mafundisho wafundishayo  siyo mazuri kwetu ,hivyo inatakiwa  kuhakikisha kile unachojifunza kama kweli ni chema mbele za Mungu na utaweza kuhakikisha kwa kusoma neno na kumruhusu roho mtakatifu atufunulie na kutufundisha.
·                   Chukua hatua ya kumng’ang’ania Mungu Kutoka 33:1-6 licha ya kuwa Musa  alimg’ang’ania Mungu si kwa kutaka mahusiano mema na Mungu bali alitaka pia ushilika na yeye,hivyo na wewe usikubali  kuondolewa au kujiondoa  mbele za Mungu  pasipo kupokea kile ambacho  umeahidiwa wewe ukipate,ng’ang’ania kwa Mungu ili ashilikiane nawe katika hali zote na majira yote na yeye  endapo utayatoa maisha yako kwake, atakupa yale yanayokufaa.
Joshua23:6 inawezekana kabisa imani zetu ni kubwa sana  lakini kama katika matendo hatufanyi inavotupasa basi imani zetu ni mfu,kwa kuwa neno la Mungu linasema imani pasipomatendo imekufa,Yakobo 2:14,17 unaposikia  neno la Mungu  epuka mizaha na kulichukulia mazoea  na uchukue hatua ya kulitendea kazi ,kwa kuwa kuna mambo huwezi kupata au hayawezi kuondoka yenyewe usipochukua hatua wewe mwenyewe,na ukichukua hatua Mungu ni mwema kwetu atatutendea na atatupa Baraka.Ameen.

Friday, February 8, 2013

UPATANISHO


Na:Cyrian Sallu.

Yohana 14:23,24 Makao ni sehemu au mahali palipotengenezwa ili kitu au kiumbe kiishi.,Neno la Mungu linasema kuwa sisi ni makao yake Yesu kristo.Yohana15:5 nyakati hizi ambazo kibiblia zinaonekana kuwa ni za mwisho wanadamu  wameamua kumfukuza Yesu ndani yao na kuruhusu Yule  roho asi ambaye ni shetani. Yohana15;7 anasisitizia umuhimu wa sisi kuwa makao  na anaahidi kutufanyia yale yote tunayomwomba tukiamini kwa jina lake atatupa.Moja ya sababu  zinazoleta shida ndani ya mioyo ya wanadamu ni kutokuwa na Mungu ndani yetu, na hili linawapata wakristo wanaojichanganya,ambao kanisani kuingia kwao ni desturi dini wanaziheshimu wakiingia kanisani wanasifu,   sadaka na michango mbalimbali wantoa lakini bado hawaamini uweza wa kriso ndani yao,na kristo mwenyewe ndani yao hayumo.
       Kupitia neno la Kristo anasema neno lake likikaa ndani yetu na yeye atakaa ndani yetu,na kupitia neno la Mungu unamruhusu Yesu mwenyewe aje kukaa na wewe.jitahidi kila neno linapokuja kwako uliruhusu likae ili kristo akae na wewe.Yohana 6:63’’Roho ndiyo itiayo uzima mwili haufai kitu’’ Ufalme wa Mungu umeenea kila mahali na  wakristo wameukataa na kuutupilia mbali ,ndiyo maana utashuhudia maajabu mengi ya kushangaza wanayafanya wakristo na siyo wapagani.Yohana 6:64.Kuamini ni kusadiki na kusadiki ni kuwa ni mmja wa waliosikia,wakristo wengi licha ya kushuhudia na kuona mambo makuu wanayotendewa na Mungu  bado  kuamini kwao kuko mbali  kwamaana hiyo wamempa nafasi shetani  ya kukaa kwao.Na kama hulisikii neno la Mungu  juwa wazi kuwa sauti utakazozisikia ni zashetani  kwa kuwa  zipo njia zilizompa uhalali wa  yeye kukaa kwako na  Mtu anaye tumkishwa na shetani anaweza kuwa mchawi hata bila yeye kujua.
,Kutoka 22:18 ,19. Maana mchawi kila akikaa anakuwa na hamu ya kuwaua wenzake  na huyu siku zote anamuhusu shetani  na ameshampa kibali cha kukaa ndani yake.Wakristo wengi licha na kumshuhudia Kristo katika maisha yao bado wanaendelea  kutambikia na kutoa kafara mbalimbali kwa shetani na maagano haya yanawapatanisha na shetani  ndiyo yanayomfanya  ibilisi apate nafasi ya kukaa ndani yetu na kutumiliki .Kumb18:22.
  Wapo manabii na watumishi ambao shetani  ndani yao ameweka pepo saba za utambuzi na wamekuwa wakiwapotosha walio wengi wakidhani kuwa ni Mungu aliyejiinua,na ili kuziepuka  roho hizi ni kuwa mtu wa kusali na kuomba ili Mungu mwenyewe ajidhihirishe kwako.Kumb 5:7,jambo linalotupoteza wakristo wengi ni  juu ya kusikiliza mafundisho na mafunuo  ya Miungu  au ya watu ambao  wanakaa na shetani na roho hizo za uasi zinakaa ndani yao.Katika maandiko Mungu anazungumza juu ya kujua mti wa mema na mbaya  ambao ni uhalali wa  kufanya uchaguzi ,ikifika mahali  ndani yako ukaanza kusikia hali ya kuwachukia watumishi bila sababu yoyote  jua ndani yako  shetani ameshapata nafasi,na kazi kubwa ni kuondoa kuamini kile Kristo alichofanya ndani yetu,na ukiona hivyo basi omba ibada ya upatanisho na Mungu ili Kristo aweze kutukuzwa ndani yako.       
Wakolosai 1:21 Neno linasema kuwa ni Yesu awezaye  kutupatanisha  na Mungu baba kwa njia ya neno lake,Wapo wakristo wengi wanafanya dhambi kwa  siri wakiwaficha wachungaji wao,wakristo wenzao na kusahau kuwa hao ni wanadamu na hawana mbingu ya kuwapeleka,na neno linatuweka wazi kuwa  Mungu huichunguza mioyo na viuno vyake na kwake hakuna siri kwa kuwa anajua  kesho na keshokutwa ya mwanadamu.Dhambi hizi  anazofanya mwanadamu ndizo zinasababisha  asipokee baraka,(Yeremia 48:7-8 )kwa maana hiyo ukiruhusu dhambi wewe mwenyewe kwa makusudi jua wazi kuwa huwezi kumwona Mungu wala kupokea Baraka kutoka kwake.
Kwa maana hiyo muombe Roho mtakatifu akukumbushe  dhambi ulizozifanya  aidha wakati unajua au hujui,ili kwamba uweze kufanya  matengenezo ya maisha yako ili uweze kujenga mahusiano mema na Mungu baba ambaye neno linasema kuwa ni mwema wa yote lakini pia ni mwingi wa rehema,na huwanyeshea mvua walimao na wasiolima,kwa maana hiyo hana ubaguzi wa mtu, ukitubu yeye ni mwema anasamehe na kusahau kabisa.Basi msihi roho mtakatifu aliyeko ndani yako aendelee kufanya mabadiliko ndani yako na Yesu mwenyewe aweze kukaa kwako milele.

Mungu akubariki sana.



:SIRI ILIYOKO KATIKA MWILI,NAFSI NA ROHO

Na Mwinjilisti Reuben





                                                                                                                                                                                        Tumwombe Mungu atujalie kuyajua mapenzi yake ,tabia yake namna  mpangilio na mapenzi yake.Watu wengi wanajuhudi katika Mungu lakini hawana maarifa ya  kumjua Mungu, kwamba tukienda kwake twende kwa namna gani ,kwamba yeye anatujua , lakini anatuona vipi hapo ndipo kuna ugumu.tunafika wakati tunamwona Mungu hawezi na hatusaidii ,kawaida huwezi kumfahamu Mungu ikiwa wewe mwenyeewe hujifahamu.  
       Huwezi kumfahamu Mungu ikiwa wewe mwenyewe hujifahamu ulivyo mbele za Mungu,kwa kuwa Mungu anasema tusafishe kabisa nafsi zetu ,mwili na roho pia kwa maana hiyo tuna sehemu kuu tatu  ambazo mwanadamu anatambulikwa kwazo nazo ni mwil,nafsi na roho. katika mwili tunajitazama  kwenye kioo kuweza kugundua kasoro tulizo nazo,lakini katia nafsi tuna misisimko hisia pamoja na utashi,lakini  katika roho tunalo neno la Mungu ambalo ndicho kioo  kinachotufanya tujitazame jinsi tulivyo na tuweze kujifahamu kuwa ni wazinzi, waongo ,wafitini ,wambea.1Wathesalonike5:23”,Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa nanyi nafsizenu miili yenu  mhifadhiwe muwe kamili bila lawama wakati wa kuja kwake bwana wetu Yesu kristo”.
     Hivyo basi walio wengi wanajua kuwa wameumbwa katika sehemu hizi tatu  lakini hawajui kazi za Mwili,Nafsi na Roho na kama hujui kazi hizo  hilo ni tatizo kwa kuwa  mwili utauchafua roho na nafsi vitashidwa kupokea Baraka  na neema za Mungu.Na endapo ukizijua kazi hizi wakati neno la Mungu likija kwako utagundua kuwa neno hili limekuja kwaajili ya mwili nafsi au roho.1Wakoritho2:10-12.Upya unaosemwa katika biblia ni neno maana anasema kwa kupigwa kwake sisi tumepona,inamaanisha tumeponyeshwa roho na nafsi na sio mwili,na kama Mungu ameshatupa inatakiwa sisi tupokee.

    Yapo Mambo Manne ambayo Unapaswa Uyafahamu.   

               Mwili unapingana na roho.wagalatia 5:17 katika maisha kuna vitu ambavyo mwili unavitaka na roho haitaki, roho inataka ila mwili hautaki,lakini ili uweze  kupata Baraka na neema za Mungu  ongozwa na neno na uifuate roho yako.Yohana6:63 .ukikubali neno la Mungu likuongoze  jua kuwa uzima wa Mungu unao, lakini ukiongozwa na mwili lazima utashidwa kwa kuwa mwili unatabia zake unania zake na na unamahitaji yake pia.tabia za mwili 1wakoritho3:1-3
-Ukiwa na tabia za mwili  huwezi kupata vitu vya rohoni,ni lazima ujichuje kuingiakatika tabia   za roho ili uweze kupokea Baraka Wagalatia5:24
,Mwili una nia yake mawazo yake,na maana ya nia ni mwelekeo wa kufikia hatma fulani kwa hiyo basi mwili kuna sehemu unataka kufika na roho pia kuna sehemu inataka kufika.Warumi8:6-8 ,nia ya mwili ni katika dhambi na nia ya roho ni  kuiona mbingu.Naomba uelewe kuwa mwili unatabia zake, kama vile ulevi uongo husuda, uzinzi na nyinginezo,na tabia za rohoni pia ni upendo, unyenyekevu,ukarimu pamoja na nyinginezo,na mtu anayeishi katika haya ana matumaini ya kufika mbinguni.
Unapokumbana na matatizo  mpaka ukahisi mifadhaiko ya kumkufuru Mungu ,jifunze  kwa waliopitia magumu na wakashinda kama vile Ayubu3:2-11.Watu wengi  tunapokumbana na wakati mgumu  ndipo tunapomwacha Mungu na kuangamia.jifunze kwa Daudi pia 1samweli30:1-4,6 Daudi alijitia nguvu  katika bwana akashinda,na wewe pia inatakiwa ujitie nguvu katika bwana.Wapendwa tuangalie jinsi ya kujitia nguvu katika bwana ili na sisi tuweze kushinda.
    
1.Tengeneza  mahusiano yako na Mungu.
     Unapokumbana na matatizo  ukawa mtu wa kulaumu ,jua unamchukiza Kristo  zaidi amini kuwa Mungu anakupenda sana zaidi ya unavyofikilia na anakuwazia mema wala siyo mabaya,hivyo jitahidi utengeneze mahusiano yako na Mungu.Warumi8:35,zab 107:19-20, waebrania4:12

2.Tafakari na kumbuka ahadi za Mungu.
      Mungu  alikuahidi nini  katika  neno lake,Kumb20:1 jua kuwa Mungu anasema na roho  wala haihusiani na milango ya  fahamu iliyo katika mwili ni tofauti kabisa.Yohana1:1…,11-12, kumb 8:18

3.Tengeneza picha  kuwa kile ulichoomba umeshapokea.
      Liamini neno la Mungu na uwe na imani ya yale uliyoomba  kuwa umeshayapokea.Warumi4:20, 10:17 jitahidi ukuze kiwango cha imani yako kiwe juu.

4.Jizoeshe kuisemesha nafsi yako.
     Jitahidi kuisemesha nafsi yako  aidha ni kuikanya au kuionya,kile ambacho Mungu anakituma kwako  kupitia neno lake hakikisha unakikubalisha katika nafsi na roho yako,elemea mwili wako  ili roho yako  iinuliwe.

5.Jenga tabia ya kufunga.
Jifunze kuwa na faragha na Mungu katika hali ya kujinyima katika mwili kwa kufunga,Kufunga kumegawanyika katika sehemu mbili,kunakufunga kuunyima mwili chakula,na pia mfungo wa aina ya pili ni kufunga nafsi yako, yaani kuinyima nafsi yako kuhitaji na kutamani vitu ambavyo mbele za Mugu ni vibovu.Na ukifunga kwa kusimama na neno la Mungu yeye ni mwema atatenda sawasawa na alivyoahidi.

 




IMANI YAKO IPO WAPI?

Na Mwinjilisti Reuben












Imani ni kuwa na hakika ya mambo ambayo hayajawa bado.Inatakiwa uione kazi,biashara na mafanikio ya maisha pasipo uhalisia kwa kufanya hivyo utakuwa umetimiza imani ya kufanikiwa hivyo utaishi maisha ya kumpendeza kwa  kutarajia yale uliyoyaamini kama atakutendea.Mungu amegawa imani kwa kila mtu pia anataka imani iendelee kukua ili uvune Baraka kwake.(Warumi 12:3),. (Waebrania 11;6) tunaelezwa kuwa Kitu ambacho kinampendeza Mungu ni Imani ,kwa maana hiyo pasipo imani hatuwezi kumpendeza Mungu.                                                                                                                                                           Kazi za shetani ni  kuiba,kuchinja na kuharibu lakini Bwana Yesu alikuja tuwe na uzima kisha tuwe nao tele,shetani anatuibia,anachinja imani na kuharibu kwa kuwa anajua akifanya hivyo hautakuwa na nafasi ya kumwamini Mungu.Imani ni kuwa na hakika ya mambo ambayo hayajawa bado,inatakiwa uione kazi,biashara na mafanikio ya maisha pasipo uhalisia ,kwa kufanya hivyo utakuwa umetimiza imani ya kufanikiwa hivyo utaishi maisha ya kumpendeza kwa  kutarajia yale uliyoyaamini kama atakutendea.Mungu amegawa imani kwa kila mtu pia anataka imani iendelee kukua ili uvune Baraka kwake.(Warumi 12:3),.

Kuna aina nyingi za imani lakini hapa tutazungumzia aina tano,ambazo mara nyingi tunakutana nazo katika maisha yetu ya kiroho na kimwili
.
01.Imani Iliyosukumiwa mbali.
 Hii ni imani iliyo tupwa ,na kuna watu wengi wanaomuona  Mungu kupitia ishara na miujiza lakini bado hawamwamini kwa maana hiyo wanaitupa imani.Paulo anasema hawa wamekabidhiwa kwa shetani ,na shetani akiwa  kwako uliyekuwa unamjua Yesu halafu ukamkana hali yako inakuwa mbaya kuzidi uliyokuwa nayo mwanzo  kwa sababu hata weza kukutendea muujiza kwa kutokumwamini kuwa yeye anaweza.

02.Imani Iliyokufa.
Hii ni imani ambayo mtu anaamini kuwa Yesu yupo lakini hatendi mema ,imani pasipo matendo imekufa,neno linahubiliwa lakini kile kilichohubiliwa huendi kukitenda lakini kwa kawaida  imani iliyo hai il itimie  lazima ulichoelekezwa na neno la Mungu inatakiwa ukifanye.Neno la Mungu linatuagiza kuwa tusiogope kwa kuwa aliye ndani yetu ni mkuu zaidi kuliko vyote,hivyo ondoka katika imani iliyokufa.

03.Imani ya Kweli.
Hii ni imani ambayo haina unafiki  wowote wala uongo ndani yake,kwasababu imani yenye unafiki ni yakuigiza wala siyo ya kweli na kuna watu ambao wanayo.Wanahofu ya kibinadamu wala hawana hofu ya kimungu.Imani ya kweli inasifa hizi;
                ­­-Inamtazama Yesu
                -Inakiri haimwonei aibu Yesu.
                 -Inatuliza moyo haina jaziba
                                                                                                                                                                                                                                                                  
 04.Imani Haba.
Ni imani ndogo sana,hii inatilia shaka juu ya mahitaji ya mwili lakini neno la Mungu linasema  atatupa vyote kwa kuwa hata tukijisumbua hatuwezi kuongeza hata urefu wa kimo cha mkono wetu.ikitokea dhoruba inatoweka.(Mathayo 8:26) na wakati wa matatizo imani hii inadhihilika kwa sabababu inamezwa na matatizo.(Mathayo 14:30) Petro alikuwa na imani lakini alipoingiza mashaka ndani yake ndipo alipoanza kuzama,jitahidi shida na matatizo uliyonayo yasikuzidi uwezo maana yanaweza kukuzamisha .
 Pia imani hii inasahaulisha mambo makuu aliyokutendea Mungu(.Mathayo16:9-10) usiwe na imani haba unapokumbana na matatizo,tafakari ni yapi uliyovushwa kwa neema  ndipo ujitie nguvu usonge mbele.

05;Imani Kuu.
(Mathayo 8;8-10), Ukitangaziwa uponyaji aminikuwa umepona,hii ndio maana ya Imani Kuu ya kutegemea neno la Mungu na kulifanyia kazi ,zifuatazo ni sifa za Imani Kuu.
-Ukiing’ang’ania huwezi kumuacha Yesu( Mathayo 15 ;21-28).
Kuna watu wakiombewa wanakuwa wepesi wa kukata tama wakati wa kusubiri majibu ya maombi yao hivyo ni heri kuvumilia kwasababu Mungu antenda kwa wakati wake kwahiyo uwe na Imani kwa neno utakalosikia kutoka kwa watumishi wa Mungu.
     Ni wajibu na haki kwa kila mkristo anayemuamini Mungu kujihoji na kufahamu imani aliyonayo ni ipi na ipo kwenye kundi lipi,je ni Imani Haba,Imani iliyotupwa au Imani kuu, na kwakufanya hivyo kutatuweka katika nafasi nzuri kwenye mahusiano kati yetu wanadamu na mungu aliye mbinguni.

Tuesday, February 5, 2013

UBATILI MTUPU


 

Na Paul Nhwani.
             
Mhubiri  12:1-11
Mfalme Suleimani anashuhudia kuwa alikuwa na mali nyingi pamoja na hekima ,lakini licha na hayo  bado akayaona yote kuwa na ubatili mtupu.licha ya hayo suleimani akaona yote ni bule usipomcha Mungu.(Mhubiri 12:13),japo alilalamika sana lakini aligundua na kusema kuwa mwanadamu lazima umche Mungu na umuhofu  MUngu pia.Suleimani  baada ya kugundua kuwa ya duinia  yanapita akaona  kuwa ni Ubatili  ni vema kumjua Mungu.
         Kwa hiyo Mfalme Suleimani anatupa maana halisi ya Ubatili kuwa  ni  kitu kisichokuwa na thamani ya kweli au ya kudumu,sasa jiulize hicho unachosumbuka nacho  kitakufikisha kwa Mungu au ndio ubatili mtupu alioona Suleimani?Maisha yetu ni mjumuisho wa mambo matatu yanayo tuzunguka ambayo ni ;MAWAZO,MANENO,MATENDO,NA MWENENDO. Tunaweza tukashidwa kufikia hatma ya mafanikio ya kumwona Mungu kutokana na mawazo maneno na matendo yetu kwa wennzetu endapo hatuwatendei yaliyo mema.kutokana na wanadamu wengi kujipenda sisi wenyewe na kuthamini mambo yetu,na kusahau kuwa Mungu ameagiza  tupendane zaidi, hata Yule ambaye kwako amekuwa ni kwazo kwako mara nyingi unaagizwa kumpenda.
                  Mambo yafuatayo yanaweza kutufanya tusifikie hatima njema ya kumwona Mungu na kujikuta tukibaki kujiita walokole bila kujua nini hatima yetu hapo baadae katika maisha ya kiroho.

01; Mienendo yetu mbele za watu na Mungu.
  Mambo haya yanaweza kuwa ubatili na kutufanya tushidwekufikia hatma njema  ya kumwona Mungu.(Mathayo 6:1-2).Mahali pengine tunafanya vitu ili tusifiwe na kuangaliwa na watu.Ukifanya  hivyo jua utapata malipo na thawabu za watu sio mbele za Mungu ,kwa hiyo tuangalie mwenenendo na tabia zetu.

02.Wanadamu kuwa  wasikilizaji wa neno na sio watendaji.
Watu waliowengi wanasikia na kuandika sana mafundisho ya neno la Mungu lakini hawayatendei kazi.Neno la Mungu ni kioo cha rohoni ambalo linatuonesha jinsi tulivyo,kwa maana nyingine linatuonesha  maisha ya mahusiano yetu na Mungu.lakini tumekuwa tukiyakimbia makusudi ya neno la Mungu juu yetu.Katika( Yakobo1:22-27). Tunaoneshwa kitu kinachosababisha tushindwe ni kuwa wasikilizaji tu na sio watendaji hivyo ni vizuri kila anaesikia neno la Mungu  kulifanyia kazi
                                                                                                                                                                                         03;Kuwa watu wa kujihesabia  haki na kuwahukumu wengine.
  Mambo ya kuhukumu  na kujihesabia haki, huo ni ubatili  mbele za Mungu .Mwinjilisti Mathayo  anasema (Mathayo 7:1-5),neno la Mungu linasema kuwa hatuna  ruhusa ya kuhukumu,na ubaya wa ubatili unakufanya  ujione muda wote  kuwa uko salama .Suleimani  alikumbushwa na Mungu,lakini kama asingekumbushwa na Mungu  yamkini hata sisi tusingepata nafasi hii ya kuoywa.
                                                                                                                                                                                                                                     04.Kuishi maisha ya uchungu na hasira
 Licha ya kuwa  watu wengi  wanatendewa mambo makuu na Mungu ,bado ndani yao  wanauchungu  wa kutokuwasamehe  wale waliowakosea.Hii inasababisha watu wasizione Baraka za Mungu na kama tutadumu katika haya ya kutokusamehe hatuwezi kufikia hatima  njema ya kumwona Mungu .Paulo anasema( Efeso 4:31-32).kusamehe kunatakiwa  ukate shauri  la kumsamehe  mtesi wako,ili ufike hatma ya kumwona Mungu.
05.Kutokuwa  na furaha katika Bwana.
Watu wengi furaha yao iko kwenye vitu,mali na katika matokeo mazuri sana,ambayo wanatendewa  na Mungu na sio katika Kristo Yesu.Hivyo basi inatupasa  kujitahidi pasipo kujali kuwa ni mzima au ni mgojwa,umepata au hujapata,umefanikiwa au hujafanikiwa,jitahidi mda wote  furaha yako iwe kwa bwana.(Wafilipi 3:1).Tufurahi katIka Bwana  na sio katika vitu, hali au matokeo mazuri.

06.Kutokuwa na upendo.
Katika maandiko matakatifu tunaagizwa kuwapenda zaidi wale  ambao wako kinyume na sisi ,lakini tumeshidwa kusimama sehemu hii zaidi  tumewahukumu wengine na  kuwaona kuwa ni waovu.Fahamu  kuwa hii inaweza ikasababisha usifikie hatma njema,Kwa kuwa Mungu ambaye ndiye tunaemwamini  yeye mwenyewe  ni upendo na alitupenda sisi kwanza.(Mathayo 5:43-45) utapata ukamilifu kwa kuwapenda  wasiokupenda  ili upate thawabu kwa Mungu wako,kwa kutokufanya hivyo  maisha yetu yatakuwa ni ubatili mtupu
.
07.Kujifanya  kuwa tunampenda  Mungu  kumbe ni uongo.
Waliowengi wanajifanya wanampenda Mungu sana lakini wanayoyafanya ni mabaya,(Mathayo 15:7-9),angalia na chunguza sana maisha yako .Mtu anaye mpenda Mungu haoni  taabu kusoma neno lake, kutoa sadaka nzuri, na kuonesha upendo kwa wenzake.hata kuweza kujitoa kwa wale wasiojiweza,  wanaohitaji kama yatima wajane,pamoja na vikongwe ,tukifanya hivyo Mungu ataonekana kwetu na tutavuna Baraka.
Na hitimisho la haya yote  (Mhubiri 12:9) jichunguze ndani ya nafsi ni lipi linaloweza kusababisha ubatili  katika maisha yako na Mbele za Mungu wako.Makusudi ya Mungu kwa wanadamu ni matatu (3)  KUMJUA MUNGU,KUMPENDA,NA KUMTUMIKIA

FAHAMU BAADHI YA TABIA ZA MWANADAMU


 

Na; Cyprian Sallu
Wapendwa katika maisha ya mwanadamu lazima kuwepo na mambo mbalimbali ambayo yanaendana na maisha yake pamoja na mazingira ili kukamilisha mfumo kamili wa maisha ya kiroho na kimwili.Hayo yote yaliyotajwa hapo yanaitwa TABIA.Tabia huleta picha kamilsi ya mtu na mfumo wake wa maisha  vilevile hujulikana haraka sana kwa jamii inayozunguka eneo husika au mtu Fulani kwa sababu wao ndio wanao kuona siku zote.Mara nyingi tumekwepa sana kutazama tabia zetu na tukajishughulisha sana na mambo ya kanisa jambo ambalo husababisha kutokea kwa dhambi.Lakini Tabia ya mtu si rahisi kubadilika  mpaka Mungu mwenyewe ambadilishe na amshuhudie kuhusu tabia yake.
Mtume Paulo alipewa neema na Mungu katika kujua tabia ya wakristo huko Effeso na Korintho alibahatika kufahamu tabia  na mwenendo wa wakristo katka kila kanisa  kupitia njia ya roho,mafunuo .na shuhuda ndio maana alisema, ‘’Sikuweza kusema nanyi kama watu wenye  tabia ya rohoni bali kama watu wenye tabia  ya mwilini kama watoto wachanga katika kristo’’.Alieleza hivyo kwa mtazamo wa tabia zetu sisi wanadamu na maisha yetu kwasababu lazima kila mtu aishi chini ya mwongozo wa neno  la mungu ili kwamba Tabia zetu ziwe za kiroho na kuwa Baraka kwa wenzetu sio vikwazo.
Kutokana na hayo tabia ikajigawa katika makundi mawili  TABIA  NZURI NA TABIA MBAYA .Lakini  pia katika hayo makundi  mawili yanajumuisha aina zifuatazo za Tabia  katika maisha ya Mwanadamu  ambazo zinahitaji utashi katika kufanya uamuzi na kuishi kwa kuepuka vikwazo nza mitego ya shetani.

Aina za Tabia:

01.Tabia ya Kurithi:

Aina  hii ya Tabia ni vigumu kuifahamu na kuitambua endapo hutakuwa mfuatiliaji na usipo vunja laana za ukoo maana hutokana na kurithi aidha kwa kupitia majina ya kurithi kutoka kwa vizazi vyetu.Katika kurithi kunaweza kuwa na Tabia nzuri au Tabia mbaya , hivyo basi ni vizuri kila mzazi kuwa makini na kufuatilia kuhusu majina na vitu ambavyo wanarithisha watoto wao.Mfano wa tabia ambazo zinaweza kurithiwa,Uchawi,Uongo,Kiburi,Hasira na Nyingine nyingi.
     Kuabudu imani za kishirikina na hata kurithishwa mikoba ya uchawi ni mmoja ya tabia za shetani                                                                                                 
Umakini unahitajika katika kuepuka aina hii ya Tabia kwasababu jamii yetu imekuwa na utamaduni wa kurithishana hasa majina  Mfano, Mtoto anaweza kuzaliwa akapewa jina la babu yake  lakini wazazi bila kufahamu na kufuatilia historia ya mwenye jina wajikuta wamempa mtoto jina bila kuvunja laana na kulitakasa jina lhilo upya ili mtoto asiweze kurithi hizo tabia  za babu yake.Ni jambo gumu sana kwa mtu asiyeamini na kufuatilia maandiko ya neno la mungu kwasababu laana imezungumzwa katika biblia kuwa inaweza kumktesa mtu bila yeye mwenyewe kujua,unaweza kuona mtu hafanikiwi au kila akifanya jambo haliendi vizuri anakimbilia kwa waganga wa kienyeji akienda kusafisha nyota kumbe siri imejificha kwenye laana ya kurithi jina la mtu wa zamani .Hivyo basi ni  vema kila mmoja kufuatilia asili ya jina lake na historia ya ukoo wake ili kuepuka kuwepo kwa tabia za kurithi bila yakujua.

02.Tabia ya Kuiga
Tabia hii inakundi kubwa la watu wambao wameathiriwa kwasababu ya mabadiliko ya mfumo wa maisha na utandawazi hasa vijana ambao  hupenda sana kuiga Tabia ,mienendo na mifumo ya maisha bila kufahamu hapo baadaye.Mara nyingi watu huiga kutoka kwa marafiki,ndugu na jamaa kwa lengo la kuwaridhisha au kujiridhisha wenyewe kwamba wanaenda na wakati lakini hawajui nini madhara ya kuiga.

1 Waebrania 13;17, anatufundisha Tabia zitupasazo kuwa nazo kuwa tuwa tii wale wanaotuongoza tena tuwaige na kufuata mienendo yao mizuri na ndio maana wakristo wengi wanabatizwa majina ya watakatifu waliopita Mfano , Petro,Musa,Paulo,Mathayo na wengine wengi.Vijana wengi wameingia katika kundi  hili la kuiga ilikuonekana wakotofauti na wengine lakini sababu kubwa ni kutokulifahamu neno lamungu pamoja na historia ya ujana wa Yesu,hivi leo kijana anaeokoka huonekana mshamba  lakini kijana aliyejiingiza kwenye kuiga mambo ya kigeni kama vikundi vya wacheza disco,walevi na wahuni anaonekana wa maana kuliko Yule aliyeko kanisani.Ni wakati wa kila kijana kujitambua na kijijengea tabia nzuri yenye misingi na misimamo ya kiroho ili kujiwekea heshima kwenye jamii na maisha yake ya kiroho yakiwa ushuhuda kwa kuutumia ujan wake vizuri bila kuiga mambo yasiyo na maana mbele za Mungu .
        Ulevi na ndoa za jinsia moja ni moja wapo ya Tabia ambazo maranyingi mwanadamu anaiga kutoka kwa mwingine
Hata jamii nzima ya kitanzania imeanza kuiga utamaduni mbovu kama ndoa za jinsia moja ambazo hazipo kwenye neno la Mungu na ni tabia ya kishetani.  Ni jukumu la watumishi wa Mungu na wazazi kuwajengea watoto na kurekebisha tabia ya kuiga ,pia kuna baadhii ya watumish nao wanaiga mambo jambo ambalo linahuzunisha na linapoteza heshima yao katika utendaji wao kwasababu hakuna Nabii wala Mtume mwenye historia ya tabia hii ya kuiga. Hivyo ni jukumu la kila mmoja kujitengenezea na kufuata tabia za kiutauwa na kuenenda  akiwa ongozwa na roho mtakatifu ili kuepuka kuiga mambo yasiyoendana na ukristo pamoja na maagizo ya Mungu wetu vile vile ni heri kuiga mambo mazuri kuliko mabaya

03:Tabia Ya Kuambukizwa:
Hii ni Tabia ya mwilini,katika amri zote mwanadamu anatakiwa ajihadhari na mawasiliano ya mtu yeyoytekidamu  ndio maana imeandikwa dhambi zote tunazofanya ni makosa lakini dhambi  ya  uzinzi na uasherate ni dhambi ya damu kuna  kuambukizana tabia kuna kuambukiza hali mbaya .Enzi hizo wayahudi wakikuta mtu anazini lazima apigwe mawe afe maana wamekwisha kuambukizana uzinzi natolea mfano uzinzi na uasherati kwasababu ni dhambi ambazo zinaambukizwa kwa kushawishiwa  mtu hawezi kufanya akiwa peke yake na zipo Tabia nyingi za kuambukizwa hivyo ni jukumu mkristo kutambua .
Ukahaba ni mmoja wapo ya tabia ya kuambukizwa












Madhara ya tabia hii inaweza kukufanya ubaki pale pale kimaendeleo unapoambukizwa dhambi au tabia yoyote ambayo sio nzuri ni vigumu kutoweka katika mfumo wako wa maisha ,mara nyingi epuka kujichanganya kwenye makundi ambayo hayana tabia kama yako kwasababu kinga ni bora kuliko tiba hivyo jikinge juu ya watu wenye uwezekano wa kukuambukiza tabia mbaya .                                                              Hizo ni baadhi ya Tabia za wanadamu tulio wengi ambao wakati mwingine tunaifanya mioyo yetu kuwa migumu kwa kutokuiga mwenendo wa mungu aliyetuumba na kuacha kuzifuata amri zake.Wakati mwingine tuna chelewa kupokea ahadi za mungu kutokana na Tabia zetu kutokumpendeza yeye katika  2 Petro2 neno linasema kwamba  bwana hachelewi kutimiza ahadi zake na anaiona Tabia yetu sisi lakini anatuvumilia na kutufundisha kupitia neno lake kuwa kama tabia zetu sio njema tufanye toba ya kweli kwani tukifa katika tabia mbaya tutaingia katika hukumu.Ni lazima kila mmoja achuchumilie kuishi maisha ya utauwa wa mungu na kujitahidi kuondoa Tabia za mwilini ambazo zimepelekea kwa wakristo wengi kuyumba katika huduma walizoitiwa na mungu.

Ili uwe na tabia nzuri au njema lazima upambane vizuri juu ya roho na mwili maana roho hushindana na mwili maana wakati mwingine roho inaamsha tama au vitu na tabia ambazo mwili hauzitaki lakini mara nyingi wakristo tumeshindwa kufanya maamuzi yaliyo sahihi na kufuata tama za mwili na kuwa maajenti wa shetani bila kujua  kutokana na kuingiwa na roho chafu kwasababu ya Tabia zetu tulizo nazo.Shetani amekuwa macho akitazama Tabia zetu hivyo akiona tabia yako mbovu anaingia kwa urahisi  vile vile jinsi tabia  yako ilivyo kutakufanya uingie jehanamu au uzimani.

Dawa Ya Tabia Mbaya:
Tabia mbaya inabadilishwa na Neno la Mungu likiingia ndani ya moyo wa mwanadamu linasafisha na kuondoa roho ngeni na Tabia zake jambo  ambalo hutokea baada ya wewe mwenyewe kuamua kumpa Yesu maisha yako na kukubali kuwa neno la Mungu ni dawa na suluhisho la shida zako.
Yesu ni dawa ya tabia mbaya ukiamini na kufuata neno lake...
Wito Kwa Wote;Wakati  wote tukumbuke mwanadamu aliumbwa na Mungu hivyo ni lazima afanye na kufuata mapenzi na amri za mungu ili asimuudhi tena tusiweke ushabiki katika kumtafuta mungu na ufalme wake lakini kwa wakati huu Wainjilisti,Wachungaji Na Wanaojiita Manabii wamekuwa na Tabia ya kujitwalia utukufu kwamba wao ndio wanamtuma Mungu na wanaponya wagonjwa, kutoa pepo kwa nguvu zao jambo ambalo halileti picha nzuri kwa watu mnao waongoza pia kuibua kiburi cha imani kati ya dhehebu na dhehebu.Inatupasa kutumika kwa moyo na kujishusha mbele za Mungu kwa kufuata maagizo na amri zake tuwaze mawazo mazuri ambayo yatatufanya tuwe na Tabia nzuri na Mungu atapata nafasi ya kukaa kwetu kutokana na mwenendo wetu mzuri .